Nembo ya VETA - Logo

Jinsi ya Kuanzisha Chuo cha Elimu ya Ufundi Stadi Nchini

MAELEZO KWA KIFUPI YA JINSI YA KUANZISHA CHUO CHA ELIMU YA UFUNDI STADI NCHINI

Chuo cha veta

1 Utangulizi

Mamlaka ya Elimu na mafunzo ya ufundi stadi(VETA) ilianzishwa chini ya sheria Na.1 ya mwaka 1994 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2006 kwa lengo la kusimamia, kuratibu na kuendesha elimu na mafunzo ya ufundi stadi nchini. VETA inasimamiwa na Bodi ya Taifa ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi (VET Board) pamoja na Bodi za Kanda (Zonal Boards) ambazo zinaendeshwa na ofisi katika kanda tisa (9) nchini.

2 Miongozo ya jinsi ya kuanzisha vyuo vya ufundi stadi

Ili kukidhi viwango vya ubora katika kutoa mafunzo VETA imeandaa miongozo ya jinsi ya kuanzisha vyuo vya ufundi stadi katika sekta kumi na mbili (12) na kila sekta ina idadi ya fani zinazomwezesha mwanafunzi kusoma na kwenda kuajiriwa au kujiajiri.

Sekta hizo ni: Ufundi Vyuma, Ufundi Magari, Ufundi Umeme, Kilimo na Usindikaji wa Chakula, Madini, Ujenzi na Uchoraji Ramani za Majengo, Hoteli na Utalii, Teknolojia ya Nguo na Ufumaji, Urembo, Usafirishaji, Biashara na Uchapaji.

Miongozo hii imeainisha viwango vinavyoweza kumsaidia mtu binafsi au taasisi katika kufanya maandalizi ya kuanzisha chuo katika sekta husika na wale wanaomiliki vyuo husaidia kufanya maboresho kwa ajili ya usajili.

2.1 Maelekezo hayo yanahusisha viwango katika maeneo yafuatayo:

i. Michoro ya majengo (kama madarasa, maabara, karakana, majiko, maktaba, stoo, vyoo na ofisi);

ii. Ujuzi na idadi ya walimu na wafanyakazi katika sekta husika;

iii. Idadi ya vifaa na zana za kufundishia katika fani husika ikiendana na idadi ya wanafunzi na walimu; na

iv. Muundo wa uongozi wa chuo.

2.2 Utaratibu

i. Mwombaji mwenye nia ya kuanzisha chuo cha ufundi stadi anatakiwa kutuma barua maombi kwenye kanda husika,

ii. Mwombaji atapewa mwongozo au miongozo kulingana na sekta anayotarajia kutoa mafunzo.Miongozo hiyo inalipiwa gharama kidogo tu.

iii. Mwombaji atajifanyia ukaguzi na kufanya maandalizi kulingana na mahitaji ya miongozo hiyo.

iv. Kama mwombaji anakidhi mahitaji ya kuanzisha chuo ataandika barua kwa Mkurugenzi wa kanda kuomba usajili wa awali;

v. Ofisi ya kanda watampatia mwongozo wa jinsi ya kuandika pendekezo la mradi (proposal).

vi. Mwombaji ataandika pendekezo la mradi na kurudisha ofisi ya kanda kulingana na maelekezo.

vii. Ofisi ya kanda watapitia andiko la mradi na kama limefikia viwango basi, ofisi ya kanda watapanga kukagua eneo husika na baadhi ya maandalizi ya kuanzisha chuo,chanzo cha fedha na vifaa.

viii. Ofisi ya kanda ikiridhika na ombi la kuanzisha chuo,basi,mwombaji atapatiwa barua ya utambulisho kwa usajili wa maandalizi (Preparatory registration). Barua hii ya usajili wa maandalizi itamwezesha mwombaji kufanya maandalizi ya kuanzisha chuo cha ufundi na katika hatua hii mwombaji harusiwi kutoa mafunzo kabisa.

Hivyo basi wadau wote wa Elimu wenye nia ya kuanzisha vyuo vya Ufundi tunaomba mtembelee ofisi zetu za kanda ili kupata miongozo ya jinsi ya kuanzisha vyuo.

Miongozo hiyo inamsaidia mwombaji kurahisiha utaratibu wa kusajili chuo kwani VETA ni washauri wakuu katika hatua zote za uanzishaji.

Ofisi za Kanda

Kwa maelezo zaidi wasiliana na ofisi zetu za kanda kwa anuani zifuatazo:

1 Kanda ya kati

Dodoma, Singida na Manyara S.L.P 2084, Dodoma
Simu:026 2322383
Nukushi:0262324120
Barua pepe: vetacentralzone@veta.go.tz

2 Kanda ya Dar es Salaam

Dar es Salaam S.L.P 40274, Dar es Salaam
Simu:026 2862651
Nukushi:026 2862651
Barua pepe: vetadsmzone@veta.go.tz

3 Kanda ya Mashariki

Pwani na Morogoro S.L.P 1955, Morogoro
Simu:023 4526
Nukushi:023 4526
Barua pepe: vetaeasternzone@veta.go.tz

4 Kanda ya Ziwa

Mwanza,Mara na Kagera S.L.P 1983 Mwanza
Simu:028 2573013/4
Nukushi: 028 2573013
Barua pepe: vetalakezone@veta.go.tz

5 Kanda ya Kaskazini

Arusha, Kilimanjaro na Tanga S.L.P 1738, Moshi
Simu:027 2754468
Nukushi:027 2754468
Barua pepe: vetanorthernzone@veta.go.tz

6 Kanda ya Kusini Mashariki

Mtwara na Lindi S.L.P 700, Mtwara
Simu:123 2333821,2333453
Nukushi: :023 2334078
Barua pepe: vetasoutheastzone@veta.go.tz

7 Kanda ya Kusini Magharibi

Mbeya,Rukwa na Katavi S.L.P 2498, Mbeya
Simu:025 2504369/72
Nukushi: :025 2504370
Barua pepe: vetasouthwestzone@veta.go.tz

8 Kanda ya Magharibi

Kigoma,Tabora na Shinyanga S.L.P 1218, Tabora
Simu:026 26048990
Nukushi: :026 2604890
Barua pepe:vetawesternzone@veta.go.tz

9 Kanda ya Nyanda za Juu

Iringa, Njombe na Ruvuma S.L.P 818, Iringa
Simu:026 2702351
Nukushi:026 2700693
Barua pepe: vetahighlandzone@veta.go.tz

Kwa mawasiliano na taarifa zaidi:

VETA Makao Makuu,
S.L. P. 2849,
Dar es Salaam, Tanzania
Baruapepe: info@veta.go.tz au pr@veta.go.tz
Simu: +255 22 2863409
Nukushi: +255 22 2863408
Tovuti: www.veta.go.tz

Mwisho (End):

Kama umependa makala hii weka maoni yako ya shukrani hapo chini au washirikishe marafiki zako wa kwenye Facebook, Instagram, Linkedin, Whatsapp, Twitter na kwenye email au mitandao mingine ya kijamii. Wasiliana nasi kama unataka kuweka kwenye blogu au website yako kwa maelekezo zaidi

If you found this article helpful please leave the comment below or share to your friends in Facebook, Instagram, Linkedin, Whatsapp, Twitter and in email or other social media. Contact us if you plan to list in your blog or website for further instructions.

Tutembelee kwenye mitandao ya kijamii hapa chini:

We offer but not limited to the following:
Business Office Documents Development, Company Registration, Business Plan Development, Curricula Development for colleges, Office Digitization Consultancy, Online Presence and Marketing Consultancy, Leadership and Management Consultancy, Constitution Development  and much more

English Form

Fomu ya Kiswahili


city, country
mji, nchi