“Tanzania Nakupenda kwa moyo wote” ni wimbo wa kizalendo kwa wazelendo wa kweli wa Tanzania. Imba wimbo huu kwa moyo wa kweli na rohoni utakuambukiza kuipenda na kujitoa kwa ajili a nchi yako pendwa ya Tanzania
- Tanzania Tanzania, nakupenda kwa moyo wote,
Nchi yangu Tanzania, jina lako ni tamu sana
Nilalapo nakuwaza wewe, niamkapo ni heri mama wee
Tanzania Tanzania, nakupenda kwa moyo wote.
- Tanzania Tanzania, ninapokwenda safarini,
Kutazama maajabu, biashara nayo makazi,
Sitaweza kusahau mimi, mambo mema ya kwetu hakika
Tanzania Tanzania, nakupenda kwa moyo wote.
- Tanzania Tanzania, watu wengi wanakusifu,
Siasa yako na desturi, ilituletea uhuru
Hatuwezi kusahau sisi, mambo mema ya kwetu hakika
Tanzania Tanzania, nakupenda kwa moyo wote.
- Tanzania Tanzania, Kaaribu wasio kwao,
Wenye shida na taabu, hukimbizwa na walowezi
Tanzania yawakaribisha, mpigane kiume chema wee
Tanzania Tanzania, heri yako kwa mataifa
- Tanzania Tanzania, watu wako ni wema sana
Nchi nyingi zakuota, nuru yako hakuna tena
Na wageni wakukimbilia, ngome yako imara kweli wee
Tanzania Tanzania, Mola awe nawe daima
Mwisho (End):
Kama umependa makala hii weka maoni yako ya shukrani hapo chini au washirikishe marafiki zako wa kwenye Facebook, Instagram, Linkedin, Whatsapp, Twitter na kwenye email au mitandao mingine ya kijamii. Wasiliana nasi kama unataka kuweka kwenye blogu au website yako kwa maelekezo zaidi
If you found this article helpful please leave the comment below or share to your friends in Facebook, Instagram, Linkedin, Whatsapp, Twitter and in email or other social media. Contact us if you plan to list in your blog or website for further instructions.
Tutembelee kwenye mitandao ya kijamii hapa chini:
English Form |
Fomu ya Kiswahili |