tengeneza pesa kwa kipaji chako

Gundua, endeleza na tengeneza pesa kwa kipaji chako

Ukurasa huu utakuonyesha namna bora ya kugundua, kuendeleza na kutengeneza pesa kutokana na kipaji ulicho nacho.

USHAURI KWA VIJANA

Je wewe unacho kitu gani tofauti na wenzako katika mji wako?
Je ni nguvu zako?
Sauti yako?
Ubunifu stadi?
Ucheshi?
Usanii?
Uongeaji?
Ushawishi?
Uhamasishaji?
Mchezaji?
Uigizaji?
Uimbaji?
Upigaji wa vyombo vya muziki?
Utumiaji wa vyombo maalumu
Kutengeneza programu za computer/simu?
Ujenzi?
Ushonaji?
Ufundishaji?
Uongozi?
Mgunduzi?
Mtaalamu wa lugha?
Mpiga picha maridadi?
Mchekeshaji?
Na zaidi na zaidi?

Kwa ngazi yeyote ya elimu yako
Sikiliza huu ushauri

Je unajua kwamba unacho hicho kipaji?
Kama ndio
Jiulize hicho kipaji ambacho ni tofauti na wengine kimekusaidia nini tangu ujue kwamba unacho?
Kama sio fanya yafuatayo:
Fanya jambo ambalo hata usipolipwa utalifurahia kulifanya kwa ustadi, ubunifu na mafanikio
Unaweza pia rudi nyuma utotoni na kujaribu kupeleleza na kuchunguza zile michezo uliyokuwa unapendelea kucheza na kufurahia. Je inaangukia kwenye sekta ipi?
Ualimu, uhandisi, sanaa, utafiti? nk
Jaribu kuyafanya yanayoendana na huo ugunduzi kila mara. Baada ya muda fulani utajikuta ukipenda sana kufanya mambo machache kuliko zile za mwanzo. Sasa unaelekea kwenye taaluma yako.
Ongeza bidii kwa kuyafanya kwa ubunifu na ari zaidi ukijizoeza kwamba motisha yake iwe ni kwenye kuifanya kwa ufanisi na sio kulipwa

Kumbuka malipo humfuata mbunifu, mchapa kazi na mpenda kazi

Ukisha jitambua kuwa sasa wewe ni wa sekta ipi na uko tofauti na wenzako katika hilo eneo, fanya yafuatayo?

Tafuta maeneo ambayo unaweza jitolea kufanya kazi bure wakati wako wa ziada

Ukijitolea itasaidia mambo matatu

  1. Kukubalika
  2. Kuibua kipaji chako
  3. Kupata fursa ya kutumia vifaa muhimu za ofisi husika zitakazosaidia kipaji chako kukua zaidi na kwa haraka

Wakati unajitolea, utajionyesha pia kwa waajiri wengi na hivyo watakuona na kuchukuliwa – Yaani umepata kazi

Kama unataka ushauri zaidi andika wasifu wako
Ambatanisha na barua yako yenye kujieleza zaidi, elezea kipaji chako kwa undani kwenda kwa

info[@]kivuyo.com (ndoa mabano)

AU tumia fomu hapo chini kwasiliana nami

Mwisho (End):

Kama umependa makala hii weka maoni yako ya shukrani hapo chini au washirikishe marafiki zako wa kwenye Facebook, Instagram, Linkedin, Whatsapp, Twitter na kwenye email au mitandao mingine ya kijamii. Wasiliana nasi kama unataka kuweka kwenye blogu au website yako kwa maelekezo zaidi

If you found this article helpful please leave the comment below or share to your friends in Facebook, Instagram, Linkedin, Whatsapp, Twitter and in email or other social media. Contact us if you plan to list in your blog or website for further instructions.

Tutembelee kwenye mitandao ya kijamii hapa chini:

We offer but not limited to the following:
Business Office Documents Development, Company Registration, Business Plan Development, Curricula Development for colleges, Office Digitization Consultancy, Online Presence and Marketing Consultancy, Leadership and Management Consultancy, Constitution Development  and much more

English Form

Fomu ya Kiswahili


city, country
mji, nchi