Kuna namna nyingi za kukaanga kuku ila leo ntakuonyesha jinsi ya kukaanga kuku kwa njia ya kisasa zaidi. Njia hii ni rahisi na inafanya kuku ziwe na ladha nzuri na pia muonekano wa kuvutia zaidi.
Mahitaji kwa kuku mmoja:
- Mayai 2
- Unga wa ngano 1/2 kilo
- Pilipilimanga kijiko 1(iliyosagwa)
- Kitunguu swaumu vijiko 2 (iliyosagwa)
- Tangawizi vijiko 2 (iliyosagwa)
- Rangi ya chakula ½ kijiko
- Limao 1
- Chumvi ½ kijiko
Maandalizi kabla ya kuanza kupika:
- Osha kuku vizuri kisha katakata katika vipande vidogo
- Pasua mayai kisha yachanganye
- Changanya unga, rangi ya chakula na mayai
Hatua za kufuata wakati wa kupika :
- Katakata kuku katika vipande vidogovidogo kisha osha
- Weka pilipilimanga, kitunguu swaumu, tangawizi,chumvi na limao kwenye kuku kisha changanya
- Chukua kuku mmoja mmoja kisha chomvya kwenye mchanganyiko wako wa mayai na unga
- Hakikisha kuku wanapata mchanganyiko huo vizuri
- Weka mafuta jikoni mpaka yachemke kisha tia kuku na uwaache waive mpaka wawe rangi ya brown
- Unaweza kutia nakshi pia kuwekea kachumbari
Mfano ya kuku waliokaangwa :
ASANTE NA KARIBU
Mwisho (End):
Kama umependa makala hii weka maoni yako ya shukrani hapo chini au washirikishe marafiki zako wa kwenye Facebook, Instagram, Linkedin, Whatsapp, Twitter na kwenye email au mitandao mingine ya kijamii. Wasiliana nasi kama unataka kuweka kwenye blogu au website yako kwa maelekezo zaidi
If you found this article helpful please leave the comment below or share to your friends in Facebook, Instagram, Linkedin, Whatsapp, Twitter and in email or other social media. Contact us if you plan to list in your blog or website for further instructions.
Tutembelee kwenye mitandao ya kijamii hapa chini:
English Form |
Fomu ya Kiswahili |