Yafuatayo ni maelezo ambayo inaweza kusaidia maofisa au watu wanaohusika na kutengeneza sera za taasisi mbalimbali. Unachotakiwa kujua kwanza ni vitu vinavyotakiwa kwenye sera. Ni vizuri pia kujua kuwa sera huandikwa ili kutatua changamoto fulani kwenye taasisi husika. Kwa hiyo muundo na maelezo ya sera inaweza kubadilika sana kulingana na muda, taasisi na mahitaji ya msingi.
Sera inaweza kuwa na kurasa nyingi ya kurasa zaidi ya mia au ikawa na kurasa chache hadi hata ukurasa mmoja tu
Tafsiri: Sera ni mkusanyiko wa taarifa zilizokusudiwa kutoa mwongozo wa jinsi gani maamuzi yapitishwe na mambo yatelekezwaje kwenye taasisi husika ili kufikia malengo tarajiwa. Mfano Sera ya fedha inatoa mwongozo wa namna gani pesa na mali za taassisi zitumike ili kufikia lengo la hizo fedha
Kumb: Sera ndogo ndogo ni vyema zikachanganywa ili kutengeneza sera moja kubwa.
Mambo muhimu yanayotakiwa:
- Utangulizi: (Maelezo mafupi ya wasifu wa taasisi ikiambatana na maono, dhima na malengo)
- Tamko la kusudio ya kuwepo kwa sera husika: (Eleza kwa ufupi kwamba sera hiyo inalenga kutatua changamoto ipi)
- Tafsiri ya maneno muhimu: (toa tafsiri au kirefu cha maneno muhimu yatakayotumika, maelezo ya vifupisho, nk)
- Maelezo ya mchakato: (Hii ndio sehemu kuu ya sera ambayo inabeba vichwa vya taarifa na sehemu zake ndogondogo ikieleza ni tendo gani lifanyika na lifanywe na nani, kwa namna gani na lini)
- Tathmini ya sera: (Elezea ni lini, nani, namna gani, na ni mambo gani hasa yanahitaji kurekebishwa ili kuboresha sera husika)
Mwisho (End):
Kama umependa makala hii weka maoni yako ya shukrani hapo chini au washirikishe marafiki zako wa kwenye Facebook, Instagram, Linkedin, Whatsapp, Twitter na kwenye email au mitandao mingine ya kijamii. Wasiliana nasi kama unataka kuweka kwenye blogu au website yako kwa maelekezo zaidi
If you found this article helpful please leave the comment below or share to your friends in Facebook, Instagram, Linkedin, Whatsapp, Twitter and in email or other social media. Contact us if you plan to list in your blog or website for further instructions.
Tutembelee kwenye mitandao ya kijamii hapa chini:
English Form |
Fomu ya Kiswahili |