Masharti Tano (5) Katika Kupata Mkopo wa Biashara

Masharti Tano (5) Muhimu Katika Kupata Mkopo wa Benki

Benki ni mkopeshaji mkubwa na mgumu kwa mazingira ya Tanzania. Pamoja na hayo benki wana masharti maalumu ambazo nazo hutofautiana kulingana na nani anakopa, anaokopa kiasi gani na kwa ajili ya biashara ipi na soko lipi. Kila benki inaweza kuwa na videzo tofautotofauti. Mikopo mikubwa huambatana na masharti lukuki tofauti na mikopo midogo. Mikopo kwa watu wenye rekodi nzuri ya kulipa ni tofauti na mkopo kwa watu wenye rekodi mbaya au ambao ndio kwanza wanaomba mkopo kwa mara ya kwanza. Mkopo kwa watu maarufu au makampuni yenye majina ni tofauti kwa watu wasio maarufu au taasisi zisizo na majina NK.

Ebu tuangalie dondoo hizi hapa chini zitakazokusaidia kujua masharti muhimu ya mabenki:

1.       Je ni biashara mpya au inayoendelea?

Biashara inayoendelea na yenye angalau miaka mitatu ina nafasi kubwa kuliko zile changa au mpya

2.       Aina ya biashara unayofanya

Biashara za kuzalisha zinanafasi kubwa kuliko zile za huduma au uchuuzi

3.       Integrity (historia safi )ya mkopaji

Historia safi ya mkopaji ya kukopa na kurudisha bila usumbufu inaongeza uwezekano mkubwa wa kupewa mkopo

4.       Dhamana na mdhamini wa mkopaji kama akishindwa kurudisha

Kwa bahati mbaya mkopaji akishindwa kurudisha kwa namna yeyote ile mkopo, je kitu gani kitafidia huo mkopo ili benki wasipate hasara AU nani atasimama kama mdhamini ili yeye ndie ashikwe endapo mkopaji atashindwa kurudisha mkopo. Aina ya dhamana na mdhamini atakayekubaliwa na benki itasaidia wewe kupata mkopo

5.     Mchanganuo wa Biashara

Mchanganuo wa biashara wenye kuonyesha mchanganuo wa kisekta, ushindani, uzalishaji, uongozi/utawala, masoko na mambo ya fedha (kwenye fedha hasa mtaji utakaohitajika, makisio ya mauzo, gharama, na faida. pia makisio ya balance sheet na cashflow itatakiwa pamoja na uwiano wa sehemu muhimu za biashara kama uwiano wa mauzo na matumizi, mauzo na mishahara, mauzo na mtaji, mauzoi na gharama ghafi, muda wa kurudisha gharama na kuanza kupata faida nk)

 

Mwisho (End):

Kama umependa makala hii weka maoni yako ya shukrani hapo chini au washirikishe marafiki zako wa kwenye Facebook, Instagram, Linkedin, Whatsapp, Twitter na kwenye email au mitandao mingine ya kijamii. Wasiliana nasi kama unataka kuweka kwenye blogu au website yako kwa maelekezo zaidi

If you found this article helpful please leave the comment below or share to your friends in Facebook, Instagram, Linkedin, Whatsapp, Twitter and in email or other social media. Contact us if you plan to list in your blog or website for further instructions.

Tutembelee kwenye mitandao ya kijamii hapa chini:

We offer but not limited to the following:
Business Office Documents Development, Company Registration, Business Plan Development, Curricula Development for colleges, Office Digitization Consultancy, Online Presence and Marketing Consultancy, Leadership and Management Consultancy, Constitution Development  and much more

English Form

Fomu ya Kiswahili


city, country
mji, nchi