Ifuatayo hapa chini ni mfano wa uandishi wa dondoo za mkutano au kikao chochote. Maoni ya namna ya kuboresha yanakaribishwa

Maelezo ya ziada

  • TDG = Kifupi cha Tumaini Development Group
  • 5 = mkutano wa 5
  • namba ya mwisho ya 1-10 ni namba ya agenda
  • Ajenda namba 1, 2, 8, 9, 10 ni agenda za lazima kwenye kikao chochote
  • Namba 8, 9 na 10 zinaweza kutofautiana lakina kichwa cha ajenda itakuwa ni ile ile

Tumaini Development Group

SLP 12908, Arusha

Taarifa ya Mkutano wa 5 wa Kikundi cha Tumaini uliofanyika Arusha Hall Tarehe 12/4/2012

Waliohudhuria

  1. Juma Hamad – Mwenyekiti
  2. Mary John – Katibu
  3. Kyuga Mwasige – Mjumbe
  4. Mwakagenda Samsoni – Mjumbe
  5. Mwanaidi Hamisi – Mjumbe
  6. Orodha ya waliohudhuria inaendelea jina moja kwa mstari mmoja

Walioalikwa

  1. Lomayani Loitore – Mwanasheria
  2. Jackson Mwita – Mshauri wa mikopo CRDB
  3. Orodha ya waalikwa inaendelea jina moja kwa mstari mmoja

Wasiohudhuria

  1. Henry Mambo – Ametoa sababu
  2. Jaffar Haji
  3. Orodha ya wasiohudhuria inaendelea jina moja kwa mstari mmoja

Ajenda

  1. Kufungua mkutano
  2. Kuthibitisha dondoo za mutano uliopita
  3. Kujadili yatokanayo na mkutano uliopita
  4. Mkopo wa CRDB – mpya
  5. Mkatabawa mradi wa maji – mpya
  6. Mikopo kwa wanachama – mpya
  7. ………………………….-mpya
  8. Mengineyo (AOB) (Kwa idhini ya mwenyekiti)
  9. Kuweka tarehe ya mkutano ujao
  10. Kufunga mkutano

TDG5-1: Kufungua mkutano

Mkutano ulifunguliwa tarehe 12/4/2012 saa 4:20 asubuhi na mwenyekiti

TDG5-2: Ajenda Zilizopitishwa

  1. Kufungua mkutano
  2. Kuthibitisha dondoo za mutano uliopita
  3. Kujadili yatokanayo na mkutano uliopita
  4. Mkopo wa CRDB– mpya
  5. Mkatabawa mradi wa maji– mpya 
  6. Mikopo kwa wanachama– mpya
  7. ………………………….-mpya imeahirishwa kujadiliwa mpaka kikao kijacho
  8. Mengineyo(Kwa idhini ya mwenyekiti)
    1. Kupokea wanachama wapya
  9. Kuweka tarehe ya mkutano ujao
  10. Kufunga mkutano

TDG5-3: Kusoma na kuthibitisha dondoo za mkutano uliopita

Dondoo za mkutano wa nne zilisomwa na kuthibitishwa na wajumbe

TDG5-4: Yatokanayo

Yafuatayo ni yatokanayo na mkutano uliopita, Maelezo zaidi kiambatanisho na. 1

  1. Katiba ya TDG

Imeazimiwa kwamba kamati ay katiba inayoongozwa na Lesom iwakilkishe rasimu ya katiba kwenye mkutano ujao

  1. Taarifa za fedha

Mkutano umeazimia kuwa marekebisho yote yaliyopendekezwa yafanyiwe kazi kabla ya mkutano ujao

TDG5-5: Mkopo wa CRDB

Mkutano umeazimia kuwa Mtunza hazina na wajumbe wawili wa mkutano wafuatilie na kujaza fomu za mkopo na kuwakilisha kwa mwenyekiti kwa ajili ya kuchukuliwa maamuzi kwenye mkutano ujao

TDG5-6: Mkataba wa mradi wa maji

Mkutano umeazimia kuwa kamati ndogo ya maji isome mkataba wa mradi wa maji kwa kushirikiana na mwanasheria na kuleta ripoti kwenye mkutano ujao

TDG5-7: Mikopo kwa wanachama

Imeazimiwa kuwa wanachama wanaotaka mkopo wa kujenga nyumba na wanakidhi masharti yote wapewe mikopo bila kuzungushwa.

TDG5-8: Mengineyo

  1. Kupokea wanachama wapya

Mkutano umeazimia kuwa zoezi la kuwaingiza wanachama wapya lisimamishwe mpaka hapo mkutano kama huu utakapotoa maamuzi mwengine

TDG4-9: Tarehe ya mkutano ujao

Mkutano umeweka tarehe 15/5/2012 saa 4.00 asubuhi kuwa ndio tarehe na sa ya mkutano ujao utakaofanyika Arusha Hall

TDG4-10: Kufunga mkutano

Mkutano ulifungwa na mwenyekiti tarehe 12 Aprili 2012 saa 11 Jioni

 

Im esainiwa na:

_______________________________________________ _______________________________________________
Mwenyekiti   Katibu